coming soon

coming soon

Friday, January 27, 2012


WAETHIOPIA KUCHEZESHA YANGA, ZAMALEK



Waamuzi kutoka Ethiopia ndiyo watakaochezesha mechi namba 7 ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Yanga na Zamalek ya Misri itakayochezwa Februari 18 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limemteua Bamlack Tessema kuwa mwamuzi wa kati kwenye mechi hiyo wakati waamuzi wasaidizi ni Yilma Knife na Mussie Kindie. Mwamuzi wa akiba (fourth official) atakuwa Waziri Sheha wa Tanzania na Kamishna wa mchezo huo ni Charles Kafatia wa Malawi.

CCM MKOA WA ILALA WAICHANGIA TWIGA STARS 26,000



CHAMA cha mapinduzi (CCM) mkoa wa Ilala kimeichangia timu ya taifa ya Wanawake 'Twiga Stars' kiasi cha shilingi 26,000 ikiwa ni mchango wake dhidi ya timu hiyo inayojiandaa na mechi yake ya marudiano ya Kombe la Afrika kwa Wanawake (AWC) dhidi ya Namibia inayotarajiwa kupigwa Jumapili katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
CCM wameungana na wadau wengine ambao wamehamasika kuichangia timu hiyo ili iweze kufanya vema katika mchezo huo
Godzila ameachia kitu cha mixed tape akiwa amemshirikisha Joti, nyimbo inakwenda kwa jina la LAKUCHUMPA. download hapo chini uisikilize ni ngoma kali sana.


DOWNLOAD HAPA

Saturday, January 7, 2012

THIERRY HENRY AREJEA EMIRATES


Thierry Henry amekamilisha uhamisho wa muda mfupi kurudi Arsenal.
The Gunners wamekamilisha makubaliano ya bima na New York Red Bulls, kwa maana Henry sasa anaweza kuanza kuichezea Arsenal kuanzia Jumatatu katika raundi ya Kombe la FA dhidi ya Leeds.
The 34-year amesajiliwa kama mbadala wa Gervinho na Maroune Chamakh, ambao watakuwa wakielekea Africa kucheza CAN na timu zao za taifa Morocco na Ivory Coast.
Henry alisema: “Ni vigumu kuwa mkweli lakini linapokuja suala la Arsenal moyo ndio utakaokuwa unaongea.
“Tangu nilipojua the plan nyuma ya usajili wangu nilikuwa sawa na kurudi Gunners. Sijarudi Arsenal ili kuwa shujaa au ku-prove kitu chochote. Nimerudi kusaidia tu.
“Watu wanabidi waelewe kwamba Chamakh na Gervinho wanaenda kucheza CAN, hivyo niliitwa kuja kujaza gap waliyoiacha.”
Henry atavaa jezi namba 12 mpaka atakapomaliza mkataba wake wa miezi miwili.
Welcome The Greatest King Theirry Henry.

RAIS DK. SHEIN AWEKA JIWE LA MSINGI NYUMBA YAMADKTARI WANORWAY.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kama ishara ya uwekaji wa jiwe la msingi Nyumba ya madaktari wa Norway Chuo cha Sayansi ya Afya Mbweni,ikiwa ni miongoni mwa shamra shamra za miaka 48 ya Mapinduzi
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akisoma maandishi ya jiwe la nyumba ya makatari baada ya kufungua pazia kama ishara ya uwekaji wa jiwe la msingi Nyumba ya madakatari wa Norway, katika Chuo cha Sayansi ya Afya Mbweni,ikiwa ni miongoni mwa shamra shamra za miaka 48 ya Mapinduzi ya Zanzibar,( kushoto) Waziri wa Afya wa Norway,Anne Crestrestom Erichsen.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Mkuu wa Chuo cha Afya ya Sayansi Hakim Bilal,alipofika chuoni hapo kuweka jiwe la msingi Nyumba ya madaktari wa Norway,ikiwa ni miongoni mwa shamra shamra za miaka 48 ya Mapinduzi ya Zanzibar